Yanga imeanza kujifua wiki iliyopita ikiwa ni maandalizi ya msimu mpya wa VPL pamoja na mchezo wa Ngao ya Jamii Agosti 23 dhidi ya Simba.
Jumla ya wachezaji 16 wako kikosini wakiendelea na mazoezi.
Lakini bado kiungo fundi Thabani Kamusoko hajarejea kutoka Zimbwabwe. Mkataba wa kiungo huyo umemalizika na tayari uongozi umeshamalizana nae juu ya kusaini mkataba mpya.
Imeelezwa wakati wowote atatua jijini Dar es salaam kusaini mkataba mpya.
Wachezaji ambao wako kambini wakiendelea na mazoezi ni wapya wanne; kipa Mcameroon, Youthe Rostand aliyesajiliwa kutoka African Lyon, beki Abdallah Hajji ‘Ninja’ kutoka Taifa Jang’ombe, kiungo Pius Buswita kutoka Mbao FC na mshambuliaji Ibrahim Ajib kutoka kwa mahasimu, Simba SC.
Wengine ni mabeki, Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Juma Abdul, Pato Ngonyani, Mwinyi Hajji Mngwali, Andrew Vincent ‘Dante’.
Viungo Geoffrey Mwashiuya, Juma Mahadhi, Said Juma Makapu, Emmanuel Martin, Yussuf Mhilu, Obrey Chirwa na mshambuliaji Amissi Tambwe.
Pia wamo Henry Okoh kutoka Nigeria na Fernando Bongnyang kutoka Cameroon ambao wanafanya majaribio.
Wachezaji ambao hawapo ni pamoja na majeruhi wawili, kipa Benno Kakolanya na kiungo Deus Kaseke; mshambuliaji Donald Ngoma amesharejea na ataanza mazoezi wakati wowote.
Beki Hassan Kessy na winga Simon Msuva wapo na kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars ambacho leo Jumatano kinakwenda Kigali, Rwanda kwa ajili ya mchezo wa marudiano na Rwanda mwishoni mwa wiki kuwania tiketi ya CHAN 2018 nchini Kenya.
Aidha Winga Simon Msuva hatakuwepo kwenye kikosi cha Yanga msimu ujao baada ya kusajiliwa na klabu ya Difaa El Jadida ya Morocco.
FAIDA ZA VITAMIN C MWILINI
*Zijue faida za kula vyakula vyenye vitamin C.* Kuna aina nyingi za vitamini na zote zina kazi mbalimbali katika miili yetu. Kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwepo kwa vitamini nyingine nyingi ambazo bado hatujazivumbua lakini ni muhimu kwa afya zetu. Tutaendele kuzitafuta kadri tutakavyo wezeshwa. Kabla ya kukufahamisha vyakula vitupatiavyo vitaminC ni vyema nikakujulisha angalau faida chache tuzipatazo kwa kuwa na vitamini C mwilini. Vitamini C husaidia mwili kutumia madini ya(Kalsiamu) chokaa na virutubisho vingine kujenga mifupa na mishipa ya damu. Bila ya kuwepo vitamini C inakuwa vigumu kwa mwili kutengeneza mifupa na mirija ya damu. Hii huwathiri sana watoto wadogo na hata walio matumboni (mimba) ambao hasa mifupa yao bado inakuwa. Uimara wa meno pia hupungua kwa kukosekana calcimu inayotumika kwa msaada wa vitamini C. Vilevile vitamini C husaidia mwili kufyonza madini ya chuma kutoka kwenye vyakula. Kuna vyakula vingine ambavyo vina madini ya chuma ambayo bila msaada wa...
Comments
Post a Comment