Yanga yaitungua Singida United 3-2
5th August 2017
Licha ya kutawala mchezo kwa sehemu kubwa, Singida United imeangukia pua baada ya kuchapwa mabao 3-2 na Yanga kwenye mchezo wa kirafiki uliopigwa kwenye dimba la Taifa.
Singida United iliuanza mchezo huo kwa kasi na kufanikiwa kupata mkwaju wa penati kwenye dakika ya kwanza tu.
Hata hivyo walikosa penati hiyo.
Thabani Kamusoko akaifungia Yanga kwenye dakika ya tano kwa mpira wa adhabu baada ya Ibrahim Ajib kufanyiwa madhambi nje kidogo ya 18.
Singida United ilisawazisha dakika tatu baadae kupitia kwa Usengimana.
United iliyokuwa 'On Fire' ikafunga bao la pili kwnye dakika ya 23 kupitia kwa Simbarashehe aliyevunja mtego wa kuotea.
Lwandamina alibadili kikosi chake chote kwenye kipindi cha pili na Yanga kufanikiwa kusawazisha kwenye dakika ya 83 kupitia mkwaju wa penati wa Amissi Tambwe.
Emanuel Martini akaifungia Yanga bao ta tatu kwenye dakika za majeruhi.
Matokeo hayo yaliibua nderemo kwa mashabiki wa Yanga huku wale wa Simba waliofurika uwanja wa Taifa kuishangilia Singida United wakitoka vichwa chini.
FAIDA ZA VITAMIN C MWILINI
*Zijue faida za kula vyakula vyenye vitamin C.* Kuna aina nyingi za vitamini na zote zina kazi mbalimbali katika miili yetu. Kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwepo kwa vitamini nyingine nyingi ambazo bado hatujazivumbua lakini ni muhimu kwa afya zetu. Tutaendele kuzitafuta kadri tutakavyo wezeshwa. Kabla ya kukufahamisha vyakula vitupatiavyo vitaminC ni vyema nikakujulisha angalau faida chache tuzipatazo kwa kuwa na vitamini C mwilini. Vitamini C husaidia mwili kutumia madini ya(Kalsiamu) chokaa na virutubisho vingine kujenga mifupa na mishipa ya damu. Bila ya kuwepo vitamini C inakuwa vigumu kwa mwili kutengeneza mifupa na mirija ya damu. Hii huwathiri sana watoto wadogo na hata walio matumboni (mimba) ambao hasa mifupa yao bado inakuwa. Uimara wa meno pia hupungua kwa kukosekana calcimu inayotumika kwa msaada wa vitamini C. Vilevile vitamini C husaidia mwili kufyonza madini ya chuma kutoka kwenye vyakula. Kuna vyakula vingine ambavyo vina madini ya chuma ambayo bila msaada wa...
Comments
Post a Comment